Tuesday, January 31, 2017

Eric Omond avitaja vigezo vitano vya kuwa Rais Bora kama Magufuli.



Yafahamu madhara ya Soda

SODA KINYWAJI KIPENDWACHO CHENYE SUMU INAYOUA POLEPOLE BILA MUHUSIKA KUTAMBUA

 

Ni hatari kwa afya ya watoto
SODA ni kinywaji kinachopendwa sana na watoto, kutokana na ladha yake tamu. Watoto ni miongoni mwa wanywaji wakubwa wa kinywaji aina ya soda. Wazazi wengi wanapotaka kuwafurahisha watoto wao huwanunulia soda bila kufahamu ina madhara yapi mwilini mwao. Katika sehemu ya pili ya makala hizi zinazotazama madhara ya soda kupitia tafiti mbalimbali zilizofanywa na wataalamu wa afya duniani, tutaangalia madhara ya soda kwa watoto wadogo.
Soda ina madhara kwa watoto kwa kuwa ina kemikali inayofahamika kitaalamu kwa jina la Caffeine. Caffeine ni aina ya kemikali inayozalishwa kwenye majani na mbegu za baadhi ya mimea. Caffeine pia huweza kutengenezwa na kuongezwa kwenye baadhi ya vyakula.

Kemikali hii ni hatari kwa kuwa huingilia mfumo wa fahamu na hivyo kufanya ushindwe kufanya kazi kama inavyotakiwa. Kwa upande mwingine Caffeine inaelezwa kuwa ni kilevi. Mtumiaji wa caffeine huchangamka na hupenda kuitumia mara kwa mara.

Baadhi ya madhara ya Caffeine iliyopo kwenye soda kwa watoto, ni pamoja na kumfanya mtoto kushindwa kufuatilia vizuri mambo ikiwa ni pamoja na masomo awapo darasani, kukosa usingizi pamoja na kuongezeka kwa mapigo ya moyo.

Utafiti uliofanywa na madaktari nchini Marekani na kuchapishwa katika jarida maarufu linalohusu afya kwa watoto la Journal of Pediatrics, unaonyesha kuwa watoto wenye umri kati ya miaka 5 hadi 7 wanaokunywa kinywaji cha soda chenye Caffeine, hulala masaa machache zaidi ya wale ambao hawatumii kinywaji chenye Caffeine.

Matokeo ya utafiti huo, yanaonyesha kuwa usingizi wa mtoto anaopata, huathiriwa na unywaji wa soda zenye Caffeine.

Tafiti nyingine zinaonyesha kuwa Caffeine ina madhara mengine zaidi kwa afya za watoto.

Utafiti uliochapishwa kwenye Jarida la Experimental and Clinical Psychopharmacology, unaonyesha kuwa unywaji wa kiasi kikubwa wa soda zenye Caffeine, husababisha kuongezeka shinikizo la damu kwa watoto wa kiume.

Watoto ambao hunywa soda kiasi cha milimita 355 kwa siku, wapo katika hatari ya kupata uzito mkubwa na kuongezeka kwa mafuta mwilini.

Vinywaji vingi vyenye Caffeine vina Kalori zisizo na kirutubisho chochote na hivyo watoto wanaovitumia vinywaji hivyo hukosa virutubisho muhimu kwa ajili ya ukuaji na maendeleo yao ya kiafya.

Tafiti mbalimbali zinaonyesha kuwa, watoto wanaokunywa soda kwa wingi (kuanzia miaka 3 hadi 8), wapo katika hatari ya kukosa Madini ya Calcium, yanayopatikana kwenye maziwa ambayo husaidia kujenga uimara wa mifupa na meno.

Tafiti nyingine zinaonyesha kuwa, unywaji wa vinywaji vyenye sukari nyingi na hasa soda ni moja kati ya sababu kuu zinazosababisha kuoza kwa meno ya watoto wakiwa bado wadogo. Ikumbukwe kuwa kiwango cha sukari kilichopo kwenye milimita 355 za soda, ni sawa na vijiko kumi vya sukari.

Caffeine huongeza uwezekano wa watoto kupata magonjwa ya moyo na matatizo katika mfumo wa fahamu, jambo ambalo wazazi hawafahamu.

Pia, kuna baadhi ya ushahidi unaoonyesha kwamba, kama una mtoto ambaye tayari ana ugonjwa wa wasiwasi (anxiety disorder), madhara ya Caffeine humfanya kuwa na hali mbaya zaidi.

Wataalamu mbalimbali waliobobea katika masuala ya afya ya umma, wanaeleza kuwa madhara ya Caffeine kwa afya ya watoto iliyopo katika soda yana athari mbaya kwa watoto.

Dk. Marcie Schneider, daktari wa watoto na mmoja wa wanakamati wa Shule ya Afya ya watoto kwenye masuala ya lishe (American Academy of Pediatrics committee on nutrition) anaeleza kuwa, Caffeine kufyonzwa tishu za mwili. Inaongeza kiwango cha mapigo ya moyo na pia huongeza shinikizo la damu.

Kwamba Caffeine husababisha mabadiliko ya joto la mwili wa mtoto, husababisha mabadiliko ya namna mtoto alivyo na kusababisha usumbufu wakati wa usingizi.

Anaielezea Caffeine kuwa humchangamsha na husababisha msisimko usio wa kawaida na pia hubadili hamu ya kawaida ya kula. Vijana wanaochipukia hupata nusu ya uzito wao wa kiutu uzima wakiwa katika umri huo. Wakiathirika na Caffeine, ulaji wao mdogo huchangia kurudisha nyuma ukuaji wao.

Dk. Nicole Caldwell, Profesa msaidizi wa afya ya watoto katika Hospitali ya Taifa ya Watoto (Nationwide Children's Hospital) Columbus, Ohio, yeye anaeleza katika utafiti wake kuwa Caffeine huathiri mfumo wa fahamu ikiwa kama stimulant.

Ubongo wa mtoto ni rahisi zaidi kuathiriwa na Caffaine tofauti na wa mtu mzima, kwa sababu humfanya mtoto kuchangamka kupitiliza. Inaweza kuwasababishia wasiwasi, matatizo ya tumbo na matatizo ya usingizi.

Caffeine husababisha kusinyaa kwa mishipa ya damu. Inachukua miligramu 4 za Caffeine kwa kilo moja ya uzito wa mwili kuongeza shinikizo la damu.

Ushahidi hauonyeshi kuwa Caffeine inasababisha kudumaa, lakini watoto wanaokunywa vinywaji vyenye Caffeine wana nafasi ndogo ya kupata Madini ya Calcium, inayohitajika mwilini.

Lakini pia, kama mtoto anayekunywa soda yenye caffeine atakuwa anaingiza kiasi kikubwa cha sukari mwilini, ambacho huweza kusababisha kuoza kwa meno pamoja na kuongezeka uzito.

Ann Condon-Meyers, mtaalamu wa masuala ya chakula na lishe (a registered dietitian) katika hospitali ya Pittsburgh, yeye anaeleza kuwa ni stimulant, hivyo ni kama kilevi.

Uzito wa mtoto hueleza ni kiasi gani cha Caffeine mwili wake unaweza kuhimili. Kwa mfano mtoto mwenye uzito wa pauni 60 anaweza kuhimili miligramu 60 za Caffeine katika kipindi cha masaa 24. Tatizo ni kuwa kuna baadhi ya vinywaji vina kiasi kikubwa sana cha Caffeine.

Madhara yake ni pamoja na kuongezeka kwa kiwango cha mapigo ya moyo, kuongezeka kwa shinikizo la damu, kuongezeka wasiwasi na upungufu wa uwezo wa kulala pamoja na homa.

Matatizo mengi yanayosababishwa na vinywaji hivi vyenye Caffeine husababishwa na kiasi kikubwa cha sukari kinachoongezwa kwenye vinywaji hivyo. Vinywaji hivi havina manufaaa yoyote kwa vile havina virutubisho. Unapokuwa na mtoto anayekunywa zaidi ya soda moja kwa siku, ujue yupo katika hatari ya kuongezeka uzito.

Mtoto anapoongezeka uzito usio wa kawaida (obesity) akiwa katika umri wa kuendelea kukuwa, anakuwa kwenye nafasi kubwa ya kuwa na tatizo hilo hata anapokuwa mtu mzima.

Unywaji wa vinywaji vyenye Caffeine haukukuwa na kujengeka kama tabia ya mtu. Binafsi napinga makampuni ya soda kutangaza bidhaa zao kwa watoto kwa kuwa si salama kwa afya yao. Nadhani ni wajanja kuweka Caffeine kwenye vinjwaji vyao kwa kuwa humfanya mtu kuwa kama teja ambaye huwaza kupata kinywaji hicho kila mara na hivyo ni kama kilevi.

Dk. Matthew Keefer, Mtaalamu wa Chakula na Lishe wa hospitali ya watoto huko Los Angels nchini Marekani, anaeleza kuwa Soda haina shida sana, lakini ina madhara mengi yasiyo ya lazima.

Anasema watoto wadogo hawahitaji Caffeine hata kidogo. Kama mtoto mwenye umri wa kati akipata kikombe cha kahawa au soda mara chache siyo jambo baya. Lakini kwa watoto wadogo huweza kusababisha kupoteza maji mengi mwilini.

“Tunatumia Caffeine kwa watoto wachanga kama wanakuwa na matatizo ya kukumbuka kupumua. Mara chache hutumika kwa watu wenye homa ya migraine, lakini zaidi ya hapo haina matumizi mengine ya kitabibu,” anaeleza Dk. Keefer.

Lakini pia inaelezwa kuwa kuna sababu kwa nini Caffeine iliyo kwenye mfumo wa kahawa ina bei ndogo. Imepewa ruzuku na makampu

ni makubwa na hivyo kuuzwa kwa bei ndogo sana.

Sababu hiyo ni kuwafanya wafanyakazi wawe wachangamfu na wenye kufanya kazi bila kuchoka. Lakini kwa watoto ni tatizo kwa sababu huwapunguzia muda wa kupumzika wakati bado wanahitaji kukuwa.

Watoto wanahitaji kulala usingizi wa kutosha. Huhitaji masaa 8 au 10 kulala usingizi wakati wa usiku, lakini wanapotumia vinywaji vyenye Caffeine hupata usingizi wa kutosha kwa shida.

Fahamu Namna mwili unavyonufaika na unywaji wa maji.


Namna mwili unavyonufaika na unywaji wa maji

Sina shaka umepata kusikia ushauri kuwa ni vema kunywa kiasi ya grasi 8 za maji kwa siku ili kusaidia mwili kudumisha kiwango sahihi cha maji mwilini na pia kufidia kiwango kinachopotea kwa njia ya mkojo, jasho na njia nyinginezo.
Sipingi kamwe ushauri huu na kimsingi nahitaji tu kuelekeza kiwango ambacho tafiti za karibuni zinapendekeza na sababu ya kunywa kiwango hicho cha maji na pia kujadili kwa uchache utendaji kazi wa maji katika mwili wa binadamu.
 Unaweza kufanikiwa kumpeleka punda mtoni tena bila usumbufu lakini kwamba atakunywa maji, inategemea na uhitaji wake kwa wakati husika, maana kwamba utafanikiwa kumlazimisha kuyanywa yale maji ni mjadala mwingine ambao sifahamu hatima yake. Sitaki watu wachukue ushawishi wangu na kukimbilia kugugumia maji bila kuwa na idadi ya sababu tena za msingi za kufanya hivyo.
Zaidi ninatamani kama ikiwa huwa unakunywa maji basi ufahamu ni kwa nini huwa unakunywa na pengine sababu hizi nitakazozijadili zinaweza kutusaidia kufahamu ikiwa vinywaji vingine vyenye vionjo vinaweza kuwa mbadala wa maji.
Chuo cha madawa nchini Marekani kinachojulikana kwa kifupi kama IOM kilichapisha utafiti wake mwaka 2004 na kueleza kuwa kila siku binadamu anapoteza lita kadhaa za maji kwa njia mbalimbali. Kwa njia ya mkojo mtu mzima anapoteza lita moja na nusu 1.5 kwa siku, kwa watu wenye kazi za kukaa (sedentary) wenye umri wa kati ya miaka 19 – 50 wanapoteza lita 3.7 wanaume na lita 2.7 wanawake kwa siku.
Na watafiti hawa walieleza kuwa njia ya kunywa maji inasaidia mwili kuongeza maji kwa asilimia 81 na hivyo kuifanya kuwa njia kuu ukilinganishwa na njia nyingine kama vile kupitia chakula ambayo ni asilimia 19 tu. Kwa sababu hiyo taasisi hii ya utafiti ilipendekeza kwamba ni vema binadamu akafidia maji yanayopotea kwa mwanaume kunywa lita 3.0 sawa na glasi13 na mwanamke lita 2.2 sawa na glasi 9. Kwa wavulana wa miaka 14 – 18 lita 2.4 na wasichana lita 2.3.
Cha zaidi ndani ya maji
Maji ni kinywaji kisicho na kalori au calorie kwa kiasi chochote kwa ajili ya mwili. Kwa sababu hiyo ni kweli kwamba unapokunywa maji hausisimui vimeng`enya kwa ajili ya kushungulika nayo kama ilivyo kwa chakula na vinywaji vingine vyenye kiwango Fulani cha calorie.
Kimsingi vinywaji vingine mbali na maji vina uwezo wa kusaidia mwili kupata kiwango cha maji lakini si kwa namna sawa na jinsi maji halisi yanafanya katika mwili.
Kwa uchache nikumbushe kwamba unywaji maji unasaidia mwili kwa kurejesha au kudumisha kiwango kinachopotea kila siku kupitia kutoka jasho, mkojo na  kupitia haja kubwa.
Maji yanasaidia mwili kusafirisha viinilishe mwilini, yanarekebisha joto la mwili, yanamsaada wakati wa ulainishaji wa chakula n.k
Maji yanasaidi afya ya ngozi na kuifanya ingae zaidi. msingi wa hili unatokana na kwamba, baadhi ya sumu zinatoka mwilini kwa njia ya ngozi. Ikiwa mwili unakiwango kikubwa cha maji basi hata sumu hizi hupunguzwa nguvu kwa sababu ya kuwa na mchanganyiko mkubwa wa maji na hivyo zinapogusa ngozi haziachi madhara makubwa kuliko mtu anayetumia maji kidogo. Yanao uwezo pia wa kuifanya ngozi isijikunje kwa kupunguza nguvu ya sumu na hili linaweza kusaidiwa na maji yanayotumiwa kuoga pia.
Utendaji kazi wa figo unategemea sana kiwango sahihi cha maji. Figo zinasafirisha kiasi ya quarts 200 za maji kila siku, zinatoa maji machafu nje na kusafirisha mkojo kwenye mirija. Kwa hivyo figo zinahitaji kiwango tosha cha maji ili ziweze kusafisha kile kisichohitajika mwilini.
Maji yanaweza kuondoa tatizo la uchovu na usingizi. Wengi hutumia kahawa kuondoa usingizi, hata hivyo usingizi na uchovu inaweza pamoja na sababu nyingine kusababishwa na kupungukiwa maji ya kutosha mwilini. Unapokunywa maji ya kutosha unaweza kurefreshi mwili na kupunguza uchovu kwa kuifanya mifumo kutenda kazi zake kwa usahihi.
Maji yanaipatia nguvu misuli. Celi za mwili hazina uwezo wa kutunza kiwango cha maji na umeme wa celi na hivyo kutegemea sana uwepo wa kiwango cha kutosha cha maji mwilini. Maji ya kutosha yanapokosekana mwilini utendaji wa celi unashuka na hivyo kuathiri nguvu katika misuli kwa sababu ya kusinyaa kwa umeme wa celi (electrolytes shrivel).

Ikiwa unywaji maji haulingani na kiwango cha mwili kupoteza tegemea upungufu wa maji mwilini. Kupitia pituitary gland ubongo unawasiliana na figo na kufahamu ni kiasi gani cha maji kinatakiwa kutolewa mwilini kwa njia ya mkojo au ni kiwango gani kinahitaji kubaki kwa ajili ya uhifadhi hii ni kwa mujibu wa mtafiti Guest ambaye ni profesa wa madawa katika chuo kikuu cha Stanford.
Kupitia njia hiyohiyo ya mawasiliano ubongo unakupatia taarifa ya uhitaji wa maji kwa njia ya kukupatia kiu. Si vema sana kusubiri kunywa maji mara baada ya kiu kwani hadi upate kiu ni kiwango cha hatari cha uhitaji wa maji mwilini ambacho ubongo unafikia kwa tathmini na hivyo kukupa kama alamu. Hata hivyo baadhi ya watu wamekuwa wakivumilia hata kiu, jambo hili la kuvumili kiu linapoendele muda mrefu huwafanya baadhi ya watu wazima kutoisikia sana katika maisha yao kwa kuwa ubongo hufikia hatua ya kuona mhusika huwa hashtuki hata kwa kumuashiria kiu kwa hivyo kwa kipindi kirefu hufika hatua na kuamua kukata ukiamini kwamba mhusika hajali hata kwa kumuashiria kiu.
Kwa sababu hizo napendekeza maji kuwa chaguao lako la kwanza dhidi ya vinywaji vingine. Kahawa au chai ni nzuri lakini ni vigumu kutenganisha cafeini iliyoko kwenye vinyaji hivyo ili kuufanya mwili uchukue maji halisi katika moja wapo ya vinywaji hivyo.
Hata hivyo kwa wanywaji wa pombe huwa mawasiliano kati ya ubongo na figo yanaingiliwa na kukatishwa na hivyo kwa kukosa msaada wa ubongo figo hujitafutia njia rahisi ambayo ni kuyatoa maji nje pindi yanapozidi na kwa wakati mwingine huyatoa kulingana na kiwango cha sumu rahisi zilizoambatana na kinywaji husika.
Kwa upande wa soda pamoja na radha ambayo inamfurahisha mnywaji lakini ukweli inauwingi wa sukari ya viwandani ambayo inaupa mwili nguvu zisizo za asili.
Kwa mujibu wa Sundaram (2001) anaeleza kwamba baadhi ya sababu zinazopelekwa mtu kupata tatizo la jiwe katika figo ni pamoja na umri kwa maana ya wazee wanapata tatizo hili zaidi ya vijana, pia jinsi inaonesha tatizo ni kwa wanaume watatu kwa wanawake wawili. Pia rangi ni zaidi kwa wazungu kuliko watu wa Asia, kwa hali ya hewa tatizo hili ni zaidi katika nchi za joto. Portis na Sundaram wanaendelea kueleza kwamba pia tatizo la kufanyika kwa mawe katika figo ni kutokana na kupungua kwa kiwango cha unywaji wa maji. Katika kupunguza hatari ya kupata tatizo hili ni vema binadamu akajijengea utamaduni wa kunywa maji ya kutosha.
Kansa ya mapafu mara nyingi inatokana na uvutaji wa sigara na moshi wa aina nyingine ambao una sumu ya coal na tar. Hata hivyo imebainika pia kwamba kunywa maji kwa kiwango kisichotosheleza mahitaji ya mwili kunachangia mtu kukabiliwa na kansa ya mapafu ( Altieri La Vecchia and Negri, 2003).
Vipo vinywaji vingi mbali na maji ambavyo vinavutia kuvitumia na hata vingine wengi wa wasiotumia vilevi huvipendekeza kwa sababu havina kilevi lakini hata hivyo vinayo madhara sawa na tumbaku, kilevi na hata sumu, vimetengenezwa kwa muonjo maridhawa wakati wa kutumia lakini vinaacha maangamizi makubwa baada ya kuvitumia kwa muda mrefu.

Ni vema ukaacha kabisa au kupunguza matumizi ya vinywaji hivi pendwa kwani havina msaada katika mwili zaidi ya madhara na badala yake unaweza anza kujizoeza kutumia maji. Maji hayana ladha ya kuvutia lakini usijali kwa sababu pindi ubongo wako utakapotambua faida nyingi za maji basi utaanza kuhisi burudani kuyatumia na baadae taratibu utaanza kuyoona yana radha kuliko hata vinywaji ulivyoviacha. Wengi wamefanya hivyo na sasa wanaishi kwa raha kwa kutumia maji tu.

Zifahamu Taratibu za Kisheria Za uanzishaji wa Biashara

TARATIBU ZA KISHERIA ZA UANZISHAJI WA BIASHARA

.....TIN inatolewa bure na mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), hakuna usumbufu katika upatikanaji, inaweza kuchukua siku 1 hadi 2. Jambo la msingi ni kwamba mlipa kodi ni lazima afike ofisi za TRA ili kujiandikisha kupitia biometric scanning inayohusisha kuchukuliwa picha, alama za vidole na sahihi....
Kupitia ukurasa huu, napenda kuufahamisha umma, hasa kwa wale wenye njozi ya kuanzisha biashara mpya kwenye ardhi ya Tanzania. Yaweza kuwa mojawapo kati ya biashara zifuatazo, yaani biashara ya mtu binafsi (sole proprietorship), biashara ya Ubia (partnership) na biashara za makampuni.
 MMILIKI BINAFSI (SOLE PROPRIETORSHIP)
Kwa wamiliki binafsi wa biashara wazawa au wageni wanahitaji kuwa na vitu vifuatavyo:
TIN
Leseni ya biashara
    -Akaunti katika benki ya biashara
     Kwa mtu ambaye sio raia wa Tanzania anapaswa kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya biashara nchini kutoka Idara ya Uhamiaji.
     TIN ni kifupisho cha maneno Taxpayer Identification Number, kwa Kiswahili namba ya utambulisho wa mlipa kodi. Ni muhimu kwa mfanyibiashara yeyote kusajiliwa na kutambulika kama mlipa kodi kupitia mamlaka ya mapato Tanzania kwani TIN ni kama uthibitisho wa mfanyabiashara kutambuliwa  na mamlaka na taasisi yoyote ya kibiashara kama vile mamlaka za miji zinazotoa vibali vya biashara pamoja na mamlaka ya mapato yenyewe. Huwezi kufanya biashara na taasisi kubwa kama vile kupewa uzabuni wa kusambaza bidhaa bila kuwa na TIN.
Baadhi ya makampuni ya mawasiliano hutoa wakala kwa watu binafsi kutoa huduma za kutuma na kupokea fedha kupitia mitandao ya simu kama vile M-PESA, TIGO PESA, AIR TEL MONEY na mitandao mingine mingi. Moja ya vigezo vikubwa vya kupewa wakala wa mitandoa hii ni kuwa na TIN. Baadhi ya wafanyabiashara wanaochukua uwakala wa kampuni za simu ama kwa kufahamu au kwa kutofahamu wameunganishwa na wakala mwingine katikati na kuwafanya wao kuwa watu wa tatu. Hii inapunguza kamisheni ambayo wakala anapata kwa kuwa kuna sehemu ya malipo inayokwenda kwa huyu mtu wa kati.
TIN inatolewa bure na mamlaka ya mapato Tanzania (TRA), hakuna usumbufu katika upatikanaji  wa TIN. TIN inaweza kupatikana ndani ya siku 1 hadi 2 kutegemeana na idadi ya maombi ambayo mamlaka imepokea kwa kipindi husika.  Mlipa kodi ni lazima afike TRA ili kujiandikisha kupitia biometric scanning inayohusisha kuchukuliwa picha, alama za vidole na sahihi.
Katika kukamilisha zoezi hili ni vema muhusika akafika moja kwa moja TRA. Siku hizi kwa ajili ya kugawana ridhiki, wapo watu wa kati wengi ambao husaidia kuwaunganisha waombaji wa TIN na TRA. Watu hawa hutumia ushamba wa watu wengi kujipatia sehemu ya kipato. Si mbaya sana kuwa nao lakini baadhi yao huwatoza wateja wao ujira mkubwa ambao hufanya zoezi la kuomba TIN kuwa na gharama kubwa wakati inaelezwa na mamlaka husika kuwa ni bure. Hata kama muombaji wa TIN atamtumia mtu wa kati ni muhimu yeyemwenyewe kuwepo ili kutoa ushirikiano atakapotakiwa kuchukuliwa picha na sahihi.
Lakini pia kufika TRA kwa mfanyabiashara mpya ni muhimu ili kuweza kupata maelezo ya ziada yanahusiana na biashara mpya na msaada wa kitaalamu. Mfanyabiashara atapata fursa ya kuwauliza maafisa wa TRA maswali kadhaa kuhusu biashara kama vile ni kwa nini vipo vyombo vingine vinavyoweza kukamata au kuzuia mzigo unaposafirishwa kutoka duka la jumla, na nini afanye ili kuepukana na usumbufu kama huu? Ni kazi ya maafisa wa TRA kukujibu maswali yote hayo bila malipo kwani ni moja ya kazi walizoajiriwa kuzifanya.
Kwa kujisajili kupata namba ya mlipa kodi inaonesha kuwa unatambua wajibu wako kama mfanyabiashara wa kuchangia pato la taifa kwa njia ya kulipa kodi. Na jambo hili ni jema tu kama alivyowahi kusema  Arthur Vanderbilt "Taxes are the lifeblood of government and no taxpayer should be permitted to escape the payment of his just share of the burden of contributing thereto." Na Richard M. Nixonaliyesema “Make sure you pay your taxes; otherwise you can get in a lot of trouble.”
 LESENI YA BIASHARA
Unatakiwa kuwa na leseni ya biashara ambayo hupatikana katika ofisi za manispaa husika chini ya Sheria ya Leseni ya Biashara Sura ya 208 kifungu cha 3 ambacho kinasema ni marufuku kufanya biashara bila kuwa na leseni halali katika eneo halali.
Muombaji wa leseni anatakiwa kufika katika moja ya ofisi ya afisa biashara katika wilaya au manispaa au mji au katika ofisi za wizara ambao ndio wanahusika na utoaji wa vibali vya biashara katika maeneo husika.
Mtu yeyote raia wa Tanzania anayo haki ya kupatiwa leseni ya biashara ili mradi awe ametimiza umri wa miaka kumi na nane (18) mwenye akili timamu ambaye hajawahi kupatikana na kosa la jinai na awe na eneo la kufanyia biashara linalokubalika kisheria. Kwa mtu ambaye sio raia wa Tanzania anapaswa kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya biashara nchini kutoka Idara ya Uhamiaji.
Baada ya kujaza fomu na viambatanisho, maombi hupitishwa ngazi zinazotakiwa kisheria – Mpango Miji na Afya. Baada ya hapo leseni hutolewa ndani ya siku moja au mbili na si zaidi.
Acaunti ya benki itamuwezesha mfanyabiashara kuhifadhi na kupokea fedha kama malipo dhidi ya washirika wake kibiashara.
2.     BIASHARA YA UBIA (PARTNERSHIP)
Kwa watu wanaotaka kufanya biashara kwa kuingia ubia ni lazima wafanye kwanza usajili kwa msajili wa makampuni BRELA na kupewa cheti cha umiliki kinachoonesha idadi na majina ya wabia katika biashara husika na asilimia za uchangiaji katika biashara.
Katika kuomba TIN wabia watatakiwa kuwasilisha nakala ya cheti cha usajili toka BRELA.
Kila mwanachama katika biashara ya ubia atatakiwa kuomba TIN, ikiwa mmoja wao alikuwa nayo hatatakiwa kuomba tena.
3.     MIFUKO YA DHAMANA
Mwenye dhamana anatakiwa kuomba usajili BRELA kwanza na kupewa cheti cha usajili kinachoonesha majina na anuani za wenye dhamana . Na pia kila mwanachama anatakiwa kuwa na TIN.
4.     MASHIRIKA YA UTU
Taasisi hizi ni lazima zipate ukubali wa kujiendesha kutoka kwa kamishina. Maombi ni vema yakaambatanishwa na nyaraka ambatanishi kutoka wizara ya mambo ya ndani.
5.     KAMPUNI
Uanzishaji wa kampuni unahitaji kusajili jina la biashara kwa Wakala wa Usajili wa Biashara (BRERA; Business Regulatory and License Agency).
Promota wa kampuni anatakiwa kuwasilisha kwa msajili kanuni za uendeshaji wa kampuni (memorandum and articles of association).
Cheti cha ushiriki katika biashara toka BRELA kitaambatanishwa wakati wa kufanya maombi ya TIN pamoja na kanuni za uendeshaji wa biashara.
UTARATIBU WA KUPATA LESENI YA BIASHARA
 Mwombaji anapaswa kujaza fomu ya maombi 9TFN kikamilifu na kuambatanisha kivuli cha:-
(i)                Jina la Biashara kama sio mtu binafsi (Certificate of Incorporation or Registration).
(ii)             “Memorandum and Article of Association” kama ni Kampuni
(iii)            Kitambulisho cha mpiga kura, Cheti cha kuzaliwa au Hati ya kiapo kuonyesha kuwa ni Mtanzania na Mgeni Hati ya kuishi nchini daraja la “A” (Residnece Permit Class “A”).
(iv)            Hati ya kiuwakili (prowess of a Honey) kama wenye hisa wote wa Kampuni wapo nje ya nchi.
(v)              Ushahidi wa maandishi kuwa ana mahali pa, kufanyia biashara (Kwa mfano hati za nyumba, mkataba wa upangishaji, risiti za malipo ya kodi za majengo au ardhi.
(vi)           Hati ya kujiandikisha kama mlipa kodi TRA (TIN).
Kwa leseni zinazodhibitiwa na Mamlaka mbalimbali , Kwa mfano (TFDA, EWURA, TAURA, CRB, TILLI) n.k lazima mwomaji kuwa na leseni husika kabla ya kuomba leseni ya biashara.
Leseni  hizi hutolewa kulingana na shughuli unayotaka kuifanya, kwa mfano kuna biashara zinalazimisha uwe na leseni kutoka Shirika la Viwango la Taifa (TBS), TFDA, Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Baraza la Wakala wa Usalama na Afya mahala pakazi (OSHA) na nyinginezo.
Utaratibu wa wajasiriamali wadogo na wa kati (smes) kuwezeshwa kupata alama ya ubora ya ‘tbs
Serikali hutenga fedha kila mwaka kwa ajili ya kuhudumia wajasiriamali wadogo na wa kati pale wanapoomba bidhaa zao wanazozizalisha wenyewe zithibitishwe ubora. Katika utaratibu huu, wapo wajasiriamali ambao husamehewa kulipa ada yoyote kwa sababu ya mitaji yao kuwa midogo.
Ili kupata msamaha huu, vigezo vifuatavyo huzingatiwa:
Mjasiriamali hutakiwa kuwa na barua ya utambulisho kutoka ofisi ya SIDO iliyo karibu. Ni vema kuhakikisha kuwa barua inafafanua vizuri na kwa kina shughuli zinazofanywa.

Kwa wale wanaozalisha vyakula huhitajika kuwa na taarifa fupi kutoka Idara ya Afya iliyo karibu na mahali pa uzalishaji au cheti cha TFDA.
Mjasiriamali hupaswa kuwa na leseni ya biashara.
 Wajasiriamali waliokwishapata leseni ya kutumia alama ya ubora hupaswa kutunza rekodi za uzalishaji na mauzo ambazo watatakiwa kuzionesha kwa wakaguzi wa TBS pindi zinapohitajika.
HATUA ZA KUPATA ALAMA YA UBORA YA ‘tbs’
1.      HATUA YA KWANZA – MAOMBI
Maombi ya uthibitishaji wa ubora wa bidhaa hufanywa na mwombaji kwenda kwa Mkurugenzi Mkuu wa TBS kwa maandishi.
Majibu hutolewa yakielezea taratibu na gharama zote.
Majibu huambatana na fomu maalum ambayo mwombaji huijaza na kuirudisha TBS ikiwa na viambatanisho vifuatavyo:

 Mtiririko wa uzalishaji wa bidhaa husika;
Mfumo wa uongozi ukionyesha kitengo cha udhibiti ubora;
Orodha ya malighafi anazotumia na mahali zinakotoka kwa kila bidhaa;
Ramani inayoelekeza jinsi ya kufika kiwandani kwako;
Baada ya hapo tarehe ya kufanya ukaguzi wa awali hupangwa.
2.      HATUA YA PILI – UKAGUZI WA AWALI
Ukaguzi wa awali hufanywa na wakaguzi wa TBS wakati kiwanda kikiwa katika uzalishaji.
Sampuli huchukuliwa na kupimwa ili kuona kama zinakidhi matakwa ya kiwango husika.

Mkaguzi huandaa taarifa kuhusu hali halisi ya kiwanda na mambo yanayostahili kurekebishwa.
3.      HATUA YA TATU – UPIMAJI
Sampuli zilizochukuliwa hupimwa katika maabara za TBS kwa kufuata kiwango husika.
 Baada ya kazi ya upimaji kumalizika, ripoti ya maabara hutolewa kwa mwombaji.
4.      HATUA YA NNE – UTOAJI WA LESENI
Maamuzi kuhusu kutoa au kutotoa leseni ya kutumia alama ya ubora hutegemea tu ripoti ya ukaguzi wa awali wa kiwanda pamoja na ripoti ya maabara.
Kimsingi ripoti zote mbili zinatakiwa kuonyesha kwamba mazingira ya uzalishaji kiwandani, mfumo wa uzalishaji na bidhaa iliyopimwa havina matatizo.
 Ikiwa sivyo basi mzalishaji hutakiwa kufanya marekebisho na baadaye mkaguzi wa TBS hutumwa tena na kuleta sampuli nyingine.
MUDA WA LESENI (VALIDITY OF LICENCE) YA ALAMA YA UBORA YA ‘tbs’
Leseni ya kutumia alama ya ubora ya ‘tbs’ hudumu kwa mwaka mmoja na huhuishwa (renewal) baada ya kuhakikisha kwamba taratibu zilizokubalika (Scheme of Inspection and Test, SIT) zinafuatwa.

Biashara za sekta ndogo zinazojihusisha na uvunaji maliasili kama vile uchimbaji madini na madini ya ujenzi (mawe, kokoto, mchanga); uvuvi; kuni na uchomaji mkaa, hazihitaji kusajiliwa na BRELA, bali vibali na leseni zake hutolewa na sekta husika.
b. Biashara katika sekta ndogo nyingine zote zinahitaji kusajiliwa na BRELA, yenye ofisi zake jijini Dar es Salaam.
c. Kuna kundi la tatu la biashara, ambazo haziko rasmi, na hizi husajiliwa kwa kupewa leseni ya Nguvu Kazi. Leseni za Nguvu Kazi hutolewa na mamlaka za serikali za mitaa chini ya Sheria ya Maendeleo ya Rasilimali Watu, kwa lengo la kuzitambua biashara ndogo ndogo. Idara ya Maendeleo ya Jamii na Idara ya Maendeleo ya Ushirika katika ngazi ya halmashauri zinahusika tu katika kusajili vikundi vya wakulima na wafanyabiashara katika maeneo yao. Kampuni zote sharti zisajiliwe na Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) au mamlaka nyingine inayoruhusiwa kisheria.
LESENI ZA VILEO
Sheria ya leseni za vileo imenyambulisha aina tisa za leseni za vileo zinazoweza kutolewa chini ya sheria hii:
Retailers On
Leseni hii humruhusu mwenye biashara kuuza pombe na kunywa eneo la biashara
RETAILERS OFF
 Leseni hii haimruhusu mtu kinywea pombe eneo la biashara bali kwa watu wanaochukua kunyewea majumbani (Take away) kama Groceries.
WHOLESALE Leseni hii ni kuuza pombe kwa jumla
HOTEL Leseni hii humruhusu mwenye leseni kuuza pombe kwa ajili ya kunywea katika eneo la biashara kwa watu waliopanga hotelini kwa wakati wowote wa mchana na usiku
 RESTAURANT Leseni hii inamruhusu mwenye leseni kuuza pombe kwa mtu yeyote anayekula chakula katika mgahawa katika muda wa saa 6.00 mchana hadi saa 8.00 mchana na saa 12.00 hadi saa 6.00 usiku.
MEMBERS CLUB Leseni hii huruhusu uuzaji wa pombe kwa kiasi chochote kwa mwanachama wa Klabu na wageni wao tu
COMBINED 4
Leseni ambazo zimeambatanishwa mhili kwa pamoja:
(a) Combined Hotel and retailers on
(b) Combined Hotel and Restaurant
(c) Combined restaurant and retailers on
TEMPORARY Leseni hii humruhusu mwenye leseni kuuza pombe katika sehemu iliyotajwa kwenye leseni mahali penye burudani, starehe au mkusanyiko mwingine kwa kipindi kisichozidi siku tatu
LOCAL LIQUOR
Class A Local Liquor
Leseni hii humruhusu mwenye leseni kutengeneza pombe za kienyeji katika sehemu iliyotajwa na kuuza kwa ajili ya kunywea sehemu ya biashara au nje ya sehemu ya biashara
Class B Local Liquor
Leseni hii humruhusu kutengeneza pombe ya kienyeji sehemu iliyotajwa na kwenda kuuzia sehemu nyingine iliyo na leseni ya kuuza pombe za kienyeji
Class C Local Liquor
Leseni hii humruhusu kutengeneza pombe ya kienyeji katika sehemu iliyotajwa kwenye leseni na kuuza kwa mwenye class D au Class E
Class D Local Liquor
Leseni hii humruhusu kuuza pombe za kienyeji katika sehemu iliyotajwa kwenye leseni kwa kunywea eneo la biashara
Class E Local Liquor
Leseni hii humruhusu kuuza pombe za kienyeji kwa ajili ya kunyewea sehemu nyingine mbali ya eneo la biashara
MASHARTI YA KUPATA LESENI
Mtu yeyote raia wa Tanzania anayo haki ya kupatiwa leseni ya Vileo ili mradi awe ametimiza umri wa miaka kumi na nane (18) mwenye akili timamu ambaye hajawahi kupatikana na kosa la jinai na awe na eneo la kufanyia biashara linalokubalika kisheria.
Kwa mtu ambaye sio raia wa Tanzania anapaswa kuwa na kibali kinachomruhusu kufanya biashara nchini kutoka Idara ya Uhamiaji.
UTARATIBU WA KUPATA LESENI
• Mwombaji hujaza fomu za maombi zinazotolewa na Manispaa
• Eneo/jingo linalokusudiwa kufanyia biashara hiyo kukaguliwa na Afisa Afya, Afisa Mipangomiji, Polisi, Afisa Mtendaji wa Kata (WDC) na Afisa Biashara wa Manispaa na hutoa maoni yao kwenye fomu husika
• Maombi hayo hupelekwa katika Malaka ya Utoaji wa Leseni za Vileo ya Manispaa kwa uamuzi
• Mwombaji ambaye maombi yake yamepitishwa hupewa Leseni baada ya kulipa ada inayotakiwa na ni lazima amekamilisha masharti ya kupata leseni hapo juu
MASHARTI YA UTUMIAJI Leseni za vileo zina masharti mengi ikiwa ni pamoja na kutouza kilevi 6 kwa watoto. Masharti mengine ni muda wa kuuza pombe na kelele za muziki.
MUDA WA KUUZA POMBE BAA (RETAILERS ON)
• Jumatatu hadi Ijumaa - Saa 12.00 jioni hadi saa 5.00 Usiku
• Jumamosi, Jumapili na Sikukuu - Saa 5.00 asubuhi hadi saa 8.00 mchana na saa 12.00 jioni hadi saa 6.00 usiku GROSARI (RETAILERS OFF)
• Jumatatu hadi Ijumaa - Saa 2.00 asubuhi hadi saa 1.00 jioni
• Jumamosi, Jumapili na Sikukuu - Saa 3.00 asubuhi hadi saa 6.00 mchana RESTAURANT LICENCE (MGAHAWA)
• Jumatatu hadi Ijumaa - Saa 6.00 mchana hadi saa 8.00 mchana na saa 12.00 jioni hasi saa 6.00 usiku
• Jumamosi, Jumapili na Sikukuu - Saa 5.00 asubuhi hadi saa 8.00 mchana na saa 12.00 jioni hadi saa 6.00 usiku MAKOSA Baadhi ya makosa chini ya sheria hii:
• Kuruhusu biashara nyingine isiyokubalika kisheria kufanyika eneo la biashara • Kuuza pombe kwa mtu mwenye umri chini ya miaka kumi na sita (16)
• Kuajiri mtu chini ya miaka kumi na sita (16) kuuza pombe
• Kuruhusu mtu mwenye umri chini ya miaka kumi na sita kukaa eneo la kuuzia pombe
• Kutoweka leseni sehemu ya wazi, ambapo itaonekana kwa urahisi na wakaguzi
• Kumruhusu/kuleta fujo katika eneo la biashara
• Kuruhusu eneo la biashara kutumika kama danguro
• Kuuza pombe muda ambao ni kinyume cha sheria
• Kufanya biashara ya pombe kwa kutumia leseni ya vileo ambao haistahili
ADHABU Mfanyabiashara anayetenda mojawapo ya makosa haya akikamatwa, atafikishwa mahakamani na akitiwa hatiani atalipa faini au kifungo au adhabu zote kwa pamoja.
UTARATIBU WA USHURU WA MALAZI (HOTEL LEVY) CHINI YA SHERIA NA. 23 YA 1972 MASHARTI YA KULIPIA HOTEL LEVY
1. Kila mmiliki wa nyumba ya wageni (Guest House) anapaswa kulipa kodi ya asilimia ishirini (20) ya malipo ya nyumba (Guest House charges) kwa mwezi husika. Wamiliki wenye mauzo yanayotozwa kodi ya zaidi ya Tshs. 40 milioni kwa mwaka hawatalipa kodi ya malazi bali watalipa Kodi ya ongezeko la tghamani (VAT)
2. Kodi iliyowekwa, italipwa kuanzia tarehe moja hadi tarehe saba ya mwezi unaofuata mauzo
UTARATIBU WA KULIPIA HOTEL LEVY
• Malipo ya Ushuru wa Malazi ni lazima yaambatanishwe na fomu ya mapato ya kila siku (fomu H.L. 1) au kitabu cha wageni, na fomu ya mapato ya kila mwezi (fomu H.L.2)
• Mmiliki wa nyumba analeta fomu H.L.1 au kitabu cha wageni pamoja na fomu H.L. 2 ambaye amekwisha jaza. Afisa anayekadiria atapitia H.L.1 au kitabu cha wageni na fomu H.L. 2 ili kuhakikisha ni sawa na kuhakikisha mmiliki amefikia vizuri asilimia 20 ya mapato ya malazi ya mwezi.
• Mmiliki akishindwa kulipa ushuru kwa muda uliopangwa, siku saba (7) baada ya mwezi husika kumalizika, atalipa nyongeza ya asilimia 25 ya ushuru unaotakiwa kulipwa, na endapo ataendelea kutokulipa adhabu (penalty) itakuwa inaongezeka kwa asilimia kumi (10) ya ushuru uliotakiwa kulipwa kila baada ya siku thelathini (30) kumalizika MAKOSA  
• Mmiliki wa nyumba ya kulala wageni kushindwa kulipa ushuru wa malazi kwa muda unaotakiwa
• Kushindwa au kukataa kuwasilisha fomu ya mapato ya kila mwezi
• Kushindwa kuweka na kutunza kitabu chenye kumbukumbu sahihi za kulala wageni
• Kushindwa kutoa risiti, hati za madai na kumbukumbu nyinginezo kama sheria inavyotaka
• Kumzuia Mkurugenzi au Mwakilishi wa Mkurugenzi katika kufanya kazi zake zilizowekwa na sheria au Kanuni za Ushuru wa Malazi
• Kushindwa kutekeleza Ilani iliyotolewa na Kamishna/mkurugenzi ya kuitwa na kuwasilisha nyaraka zinazohusu nyumba yake ya kulala wageni
• Kutoa taarifa ya uongo kwenye kumbukumbu yeyote inayotumika kwa ajili ya kudanganya au kushindwa au kukataa kujibu maswali vizuri kwa Afisa wa Serikali aliyepewa madaraka na sheria hii ADHABU
• Mmiliki atakayetenda mojawapo ya makosa yaliyotajwa hapo juu atalipa faini isiyopungua Tshs. 50,000.00 kwa Mkruugenzi wa Manispaa na isiyozidi Laki tano (500,000.00) Mahakamani akipatikana na hatia.
• Mmiliki anayekwepa kulipa Ushuru wa Malazi kwa makusudi akikamatwa na kutiwa hatiani atalipa faini isiyozidi shilingi milioni mbili (2,000,000.00)
Hata hivyo kila halmashauri ya wilaya na miji zina utaratibu wake ambao ni vema mfanyabiashara akachukua hatua katika kufahamu ili kuepuka uvunjaji wa kanuni za uendeshaji wa biashara na kuepuka adhabu.

Hatimaye Matokeo ya Kidato Cha nne-2016 Yatoka,


 

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

CSEE 2016 EXAMINATION RESULTS ENQUIRIES



CLICK ANY LETTER BELOW TO FILTER CENTRES BY ALPHABET
A
B
C
D
E
F
G
H
I
J
K
L
M
N
O
P
Q
R
S
T
U
V
W
X
Y
Z






Kama Link hii haifunguki kwa haraka ufunguapo,Endelea kuijaribu bado ni nzito kutokana na mtandao.